Featured

    Featured Posts

WASAKATONGE

UCHAMBUZI  WA  FASIHI SIMULIZI

WASAKATONGE


MWANDISHI: MOHAMED S KHATIBU
WACHAPISHAJI: OXFORD UNIVERSITY PRESS
MWAKA: 2003


FANI

JINA LA KITABU
Wasakatonge ni jina sadifu kulingana na yale ambayo mwandishi ameyaeleza katika kitabu. Mashairi mengi aliyoyaelezea mwandishi yanawagusa wasakatonge, walalahoi, wanyonge na watu wa tabaka la chini kwa ujumla wake. Katika kitabu kuna shairi la “Wasakatonge” shairi hili linabeba picha halisi ya jina la kitabu. Anazungumzia juu ya hali ngumu ya kimaisha ya watu hawa. Kazi wanazofanya ni ngumu na ujira kidogo. Anaona kuwa hali hii ya baadhi ya wananchi sababu yake ni viongozi wasaliti ambao waliwaweka wenyewe madarakani. Sio tu kwamba jina hili limesadifu tu yaliyo katika kitabu bali pia hata katika jamii. Mambo ya unyanyasaji na ukandamizwaji wa tabaka la chini yameoneshwa makusudi ili jamii iweze kurekebika na wanaohusika na hili wachukue hatua mara moja kupunguza idadi ya walahoi nchini.
FANI
MUUNDO
Mwandishi ametumia miundo ifauatayo:

Tathlitha
Mfano wa mashairi yaliyotumia muundo huu ni “Nilinde”, “Tutabakia wawili”, “Itoe kauli yako”, “usiku wa kiza”, “Sikujua”.

Sabilia
Mfano wa mashairi ni “Waso dhambi”, “Sikuliwa sikuzama”, “Madikteta”,“Si wewe?”,“Vinyonga”

Tarbia
Mfano ni shairi la “Mahaba”, “Machozi ya dhiki”, “Mcheza hawi kiwete”, “Sivui maji mafu”.

MTINDO
Mwandishi ametumia mtindo wa kisasa na wa kimapokeo.
Katika mashairi ya kisasa mwandishi ametumia ubunifu zaidi kwani yapo baadhi ya mashairi ambayo ameweka kiitikio mwishoni mwa ubeti mfano shairi la “Sikujua”, “Tutabakia wawili” “Jiwe si mchi”. Pia kuna mashairi mengine kama vile “Wanawake wa Afrika” “Nuru ya tumaini” “Hatuna kauli”.
Mashairi ya kimapokea mfano, “Mahaba”, “mcheza hawi kiwete” “Sivui maji mafu” na mengine.

MATUMIZI YA LUGHA
Tamathali za semi
Tashibiha
“lnanuka kama ng’onda” – “Kansa”
“Ni ndwele kama kansa” – “Kansa”
“Tubaki chanda na pete, kama udi na ambari”- “Nilinde”
“Hubakia kama wanga, mahepe tunachagawa” – “Nilichelewa kupendwa”
“Vimeenea Vinyonga                                                        
kama vile vimeleya” – “Vinyonga”

Sitiari
“Tabaki chanda na pete” – “Nilinde”
“Usijigeuze Popo” – “Itoe kauli yako”
“Ndwele ni maskini” – “Tiba isiyotibu”
“Mate si baragumu”- “Mtemea mate mbingu”
“Uchoyo ni sumu” – “Pendo tamu”

Tashihisi
“Inaumwa Afrika” – “Tiba isotibu”
“Radi yenye chereko” – “Afrika”
“Pendo lenye tabasamu” – “Pendo tamu

Mubaalagha
“Pendo tamu kama letu duniani hulikuti” – “Pendo tamu”.
Mbinu nyingine za kisanaa

Takriri
Mfano “nilikesha”- “nilikesha”
“Buzi” – “Buzi lisilochunika”
Matumizi ya semi

Misemo
“mcheza hawi kiwete, ngoma yataka matao” – “Mcheza hawi kiwete”

Ujenzi wa taswira
“Vinyonga” – “viongozi wasaliti” – “vinyonga”
 “Punda” – “Sikujua”.
“Chui na Simba”- “watu wenye mamlaka” – “miamba”
“Bundi” – wakoloni wanyonyaji” – “Bundi”
“Vindama”- “nchi zinazoendelea” – “fahali la dunia”.
“Fahali la dunia” – “nchi za ulaya”
author

Author Name

Author Description!

Get Free Email Updates to your Inbox!

www.CodeNirvana.in

nn

  • CSS3 all images appearing slideshow example test questions
  • jQuery vertical em  embedphoto behind
  • HTML5 full screen iphone  thumbnail with images
  • HTML continuous with controls  download photo
HTML5 image carousel

Inaendeshwa na Blogger.
Copyright © www.elimu.cf | LOCATION TANZANIA PRIVATE SITE